NGUZO ZA KIISLAMU
Dini hii ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo tatu za msingi, ambazo ni:-
1. UISLAMU, ambao huu umejengwa juu ya nguzo tano kama zifuatavyo:-
Shahada mbili
Kusimamisha swala tano
Kutoa zakah
Saumu ya Ramadhani
Kuhiji Makah (kwa mwenye uwezo).
2. IMANI nguzo hii ya pili ya dini ya Kiislamu inajengeka juu ya nguzo sita zifuatazo:-
i. Kumuamini Allah
ii. Kuwaamini malaika wa Allah.
iii. Kuviamini vitabu vya Allah.
iv. Kuwaamini mitume (wote ) wa Allah.
v. Kuamini siku ya mwisho.
vi. Kuamini qadari ya Allah (ya kheri au ya shari) kuwa inatoka kwa Allah).
3. IHSANI. Nguzo hii ya tatu inaundwa na nguzo hii:-
Kumuabudu Allah kama unamuona Kama humuoni yeye anakuona wewe.
Huu
kwa muhtasari ndio Uislamu, dini na mfumo sahihi na kamili wa maisha
kwa wanadamu wote waliochaguliwa na Allah Mola Muumba wao:
“………LEO NIMEKUKAMILISHENI DINI YENU NA KUKUTIMIZIENI NEEMA YANGU NA NIMEKUPENDELEENI UISLAMU UWE DINI YENU ………….” (5:3)
Elewa
na ufahamu kwamba kuishi nje ya dini hii ni kulikana umbile lako kwani
UISLAMU NI HAKI YAKO YA KUZALIWA uliyopewa hadiya (zawadi) na
Mola Muumba wako.
Endelea kuungana nasi katika mafundisho yajayo.............

No comments:
Post a Comment